Showing posts with label Stories. Show all posts
Showing posts with label Stories. Show all posts

Thursday, April 23, 2015

JAMAA APIGWA NA MKEWE KISA MCHEZO WA KUBET

Jamaa mmoja wa pande za Magomeni siku ya juzi alijikuta akipata mkong'oto wa hatari  kutoka kwa mkewe baada ya kisa kuwa, jamaa huwa anaenda kushinda kwenye kubet tuuu bila ya kumwachia mkewe hata hela ya chakula. Hata hivyo kwa habari za majirani wanadai kwamba walishindwa kumtoa jamaa kwenye mkong'oto wa mkewe kwa sababu, mke wa jamaa ananyanyua vyuma hivyo nao wameogopa kuwa nao wangepata mkong'oto kutoka kwa mwanadada huyo.

Friday, March 6, 2015

MAMA MWENYE NYUMBA AMDUNDA BABA MWENYE NYUMBA

duuh!!! uswahilini kuna vituko. Mama mwenye nyumba mmoja wa pande za kitaa fulani humu dsm, amempiga mumewe (baba mwenye nyumba) baada ya kukanyaga sehemu aliyokuwa anapiga deki. Watu walioona tukio hilo waliamua kupiga simu polisi, mara moja nao polisi waliwasili kwa muda maalum. Mazungumzo kati ya mama huyo na polis hao yalikuwa hivi:

POLISI; Mama mwenye nyumba, tumepigiwa simu na watu waliokuona una mpiga mume wako (baba mwenye nyumba) kwa hiyo unaweza kutuambia sababu ya kumpiga mume wako??

MAMA MWENYE NYUMBA: Ndio nimempiga kwa sababu amekanyaga sehemu niliyopiga deki ambayo ilikuwa haijakauka.

POLISI: Bhas mama una makosa hivyo unahitajika kituoni.

Mama mwenye nyumba akawa hajajibu. Bhas polisi walimpigia mkubwa wao na kumwambia yaliyotokea.
Mazungumzo ya polisi na mkubwa wao yalikuwa hivi:

POLISI: Afande tupo huku kwenye tukio maeneo ya uswahilini huku, mama mwenye nyumba amempiga mumewe.

AFANDE: Kampiga mumewe kisa nini??

POLISI: Kampiga kisa alikanyaga sehemu aliyopiga deki ambayo ilikuwa haijakauka.

AFANDE: Mmeshamkamata?

POLISI: Hapana afande.

AFANDE: Kwa nini sasa?

POLISI: Tunaogopa kupigwa afande, hivyo tunangojea pakauke ndo tumkamate.

Saturday, February 28, 2015

MTOTO AWAGOMBANISHA WAZAZI WAKE

Mtoto mmoja wa pande za kishua a.k.a Masaki siku ya juzi aliwagombanisha wazazi wake baada ya kuagizwa na mama yake kumpigia simu baba yake. Mazungumzo hayo kati ya mama na mtoto yalikuwa hivi:

MAMA: Mwanangu embu mpigie simu baba yako kwa sababu, muda mfupi uliopita alinipigia na kuniambia kuwa nimpigie nikiwa nimeshamaliza kupika chakula.

MTOTO: Sawa mama.

Bhas yule mtoto akafanya kama alivyoambiwa na mama yake. Mara mtoto akatoa majibu kwa mama yake.

MTOTO: Mama!!! nimempigia baba, ila hajapokea yeye.

MAMA: khah!! amepokea nani mwanangu??

MTOTO; Amepokea mwanamke mama.

MAMA: Bhas mwanangu hilo swala niachie mimi.

Bhas yule mama na mtoto wake wakaendelea kula chakula. Baada ya muda kidogo wakasikia mlinzi akifungua geti na sauti ya gari. Bhas yule mama alienda mlangoni huku akiwa ameshikilia mwiko, upawa, sufuria, frampeni, vijiko na bila kusahau uma.

Mara baba wa mtoto akafungua mlango, lakini kabla ya kumalizia kuingia ndani, baba wamtoto alishangaa anapigwa na mwiko, upawa , sufuria na vinginevyo huku mama wa mtoto akisema, "utanieleza leo, aliyepokea simu yako ni nani". Mara mama akamwita mtoto wake,:

MAMA: Mwanangu embu mwambie baba yako kuhusu yule mwanamke aliyepokea simu alikuambiaje?

MTOTO: Baba, Yule mwanamke aliyepoke simu alisema kwamba, " Namba unayopiga kwa sasa haipatikani, tafadhali jaribu tena baadae.

Bhas yule mama akachoka akawa hoii na baba wa mtoto nae akawa hajasema kitu.




ASANTE KWA KUSOMA STORI HII AMBAYO IMeKUFURAHISHA. TAFADHALI ENDELEA KUPITIA www.justbehappy005.blogspot.com KWA STORI NYINGINE ZAIDI.


ASANTENI